top of page
Search

Usingizi

  • Writer: Neema Komba
    Neema Komba
  • Oct 14
  • 1 min read
ree

Wanikosesha usingizi

Tanzania ya siku hizi,

Uloikata mizizi

Na kusahau misingi

Uliyosimika siku nyingi

 

Ndotoni unanijia

Kwa kilio na hasira

‘Nisuta kukosa dira

Na kunidai uhuru

Ulopigania siku nyingi

 

Wanikumbusha amani

Haiji bila ya haki

Na ukombozi wetu thabiti

Haukuja bila ya dhiki

Na damu za wafianchi

 
 
 

1 Comment


Gloria D. Gonsalves
Gloria D. Gonsalves
Oct 30

Inatukosesha usingizi wengi. Ni ngumu kujikumbusha penye giza mwangaza unakuja. Mungu ibariki Tanzania yetu pendwa na watu wake.

Like
bottom of page