Usingizi
- Neema Komba

- Oct 14
- 1 min read

Wanikosesha usingizi
Tanzania ya siku hizi,
Uloikata mizizi
Na kusahau misingi
Uliyosimika siku nyingi
Ndotoni unanijia
Kwa kilio na hasira
‘Nisuta kukosa dira
Na kunidai uhuru
Ulopigania siku nyingi
Wanikumbusha amani
Haiji bila ya haki
Na ukombozi wetu thabiti
Haukuja bila ya dhiki
Na damu za wafianchi






Inatukosesha usingizi wengi. Ni ngumu kujikumbusha penye giza mwangaza unakuja. Mungu ibariki Tanzania yetu pendwa na watu wake.